Skip to main content

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo amesema zoezi la sensa ya watu na makazi si la kisiasa, bali ni la m…

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo amesema zoezi la sensa ya watu na makazi si la kisiasa, bali ni la maendeleo ya watanzania wote hivyo wajitokeze kuhesabiwa.

Chongolo ametoa kauli hiyo hii leo katika kata ya Kaloleni wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, alipozungumza na wanachama wa CCM wa Shina namba mbili.

Akihamasisha wananchi kushiriki sensa ya watu na makazi inayofanyika tarehe 23 mwezi huu Chongolo amesema, sensa sio suala la kisiasa na kuonya wanachama wa CCM na wananchi wasikubali kuhadaiwa.

Chongolo yupo katika ziara ya kukagua uhai wa Chama Cha Mapinduzi mkoani Kilimanjaro.

Pia anatumia ziara hiyo kuhamasisha wananchi kushiriki katika zoezi la sensa ya watu na makazi.




Title of the document



The post Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo amesema zoezi la sensa ya watu na makazi si la kisiasa, bali ni la m… appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/43008/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT