Skip to main content

Bwawa la kuzalisha umeme Ethiopia lafunguliwa licha ya tetesi za Misri na Sudan

Ethiopia imesema mtambo wa pili kwenye bwawa lake la kuzalisha umeme ambalo limekumbwa na utata kwenye mto Blue Nile umeanza kufanya kazi.

Bwawa hilo kubwa lililogharimu kiasi cha dola bilioni 4, limesababisha mgogoro mkubwa kati ya nchi hiyo, Misri na Sudan ambazo zinategemea sana maji yam to Nile.

Bwawa hilo linatarajiwa kuzalisha zaidi ya megawati 5000 za umeme litakapokamilika.

Licha ya mazungumzo ya mara kwa mara, hakuna makubaliano yamefikiwa kati ya nchi hizo tatu.

Cairo na Khartoum zinataka makubaliano juu ya matumizi ya maji ya mto Nile na namna ya kukabiliana na ukame endapo utataokea. Nchi hizo pia zimekasirishwa na Ethiopiakwa vile ilianza kujaza maji kwenye bwawa hilo kabla ya makubaliano kufikiwa.

Ethiopia ilianza kuzalisha umeme kutoka kwenye bwawa hilo mwezi Febrauri mwaka huu.

Ujenzi wake ulichukua zaidi ya mwongo mmoja.

The post Bwawa la kuzalisha umeme Ethiopia lafunguliwa licha ya tetesi za Misri na Sudan appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/2PbEWqw

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT