Skip to main content

Blinken: nchi zenye nguvu zingeiga mfano kutoka kwa Russia na kushambulia zingine

Blinken alikuwa akizungumza na waandishi wa habari nchini Afrika kusini, ambapo alikutana na waziri wa mambo ya nje wa Afrika kusini Naledi Pandor, katika ziara yake ya nchi tatu za Afrika, ambapo pia atatembelea Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo na Rwanda.

Amesema kwamba endapo ulimwengu utaruhusu nchi zenye nguvu duniani kuvamia nchi ndogo itakuwa jambo la kawaida kwa nchi nyingine kufanya hivyo sio tu Ulaya bali kote duniani, bila kuwajibishwa.

Blinken amesema kwamba Marekani inatambua kwamba ni muhimu kuiwajibisha Russia kutokana na uvamizi kwake Ukraine kwa sababu uvamizi huo unatishia misingi ya hali kote duniani.

Russia ilivamia Ukraine Februari tarehe 24 katika kile inakitaka kama operesheni maalum ya kijeshi ili kuwalinda watu wanaozungumza kirusi nchini Ukraine.

Waziri wa mambo ya nje wa Afrika kusini amesema kwamba hakuna mtu yeyote anaunga mkono vita vinavyoendelea Ukraine lakini mifumo ya sheria ya kimataifa inaonekana kutekelezwa kwa upendeleo, akitaka hatua kama hizo kuchukuliwa ili kuangazia yanayoendelea Palestina

The post Blinken: nchi zenye nguvu zingeiga mfano kutoka kwa Russia na kushambulia zingine appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/44767/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT