Skip to main content

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson ana wakati mgumu kutetea wadhifa wake kisiasa

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson alikuwa akipigania uhai wake wa kisiasa siku ya Jumanne baada ya Waziri wa Fedha Rishi Sunak, na waziri mwingine mwandamizi kujiuzulu ghafla kutokana na kashfa ya hivi karibuni iliyoharibu utawala wake.

Ndani ya muda wa dakika kadhaa kwa kila mmoja Sunak na Waziri wa Afya Sajid Javid walimtumia Johnson barua za kujiuzulu ambazo zililenga uwezo wake wa kusimamia utawala unaofuata viwango.

Akiashiria nia yake ya kubaki madarakani kwa muda mrefu kadri iwezekanavyo Johnson alimteua haraka mfanyabiashara wa zamani Nadhim Zahawi hivi sasa ni Waziri wa Elimu kama waziri wake mpya wa fedha.

Wakati huo huo Steve Barclay aliteuliwa Februari kuweka nidhamu katika utawala wa Johnson alihamishwa kwenda kitengo cha afya. Kujiuzulu kulikuja huku Johnson akiomba radhi kwa kumteua mbunge kuhusika katika kutoa huduma ya uchungaji kwa chama chake hata baada ya kuelezwa kuwa mwanasiasa huyo amekuwa akilalamikiwa kuhusu unyanyasaji wa kingono.

The post Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson ana wakati mgumu kutetea wadhifa wake kisiasa appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/RKQ7Jz4

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT