Skip to main content

Watu watano wauawa na wanamgambo mashariki mwa DRC

Shambulio hilo la waasi wa Alliance Democratic Forces (ADF) la Jumamosi usiku linajiri baada siku mbili tu baada ya kufanyika shambulio kama hilo katika mkoa jirani na kusababisha vifo vya watu 13.

“Majira ya saa tatu usiku, walishambulia kijiji cha Busiyo katika mkoa wa Ituri, na kuchoma nyumba kadhaa, Jacques Anayeyi, kiongozi wa baraza la vijana, ameiambia AFP Jumapili.

Amesema watu watano waliuawa, wakiwemo watoto wanne kutoka familia moja ambao walichomwa hadi kufa ndani ya nyumba yao.

Ameongeza kuwa wanavijiji watano walijeruhiwa na darzeni ya wengine kutekwa nyara.

Shambulio hilo limetokea wakati viongozi walikuwa wanatarajia kuwarejesha makwao wakazi baada ya kuzuka kwa machafuko katika eneo hilo.

“Tulikuwa tumewatayarisha wakazi warejee makwao, lakini kutokana na shambulio jingine la magaidi wa ADF, kurejea itakuwa vigumu,” amesema Faustin Babanilao Mboma, kiongozi wa eneo la utawala la Banyali Tchabi, akithibitisha vifo hivyo.

Waasi hao walishambulia kijiji jirani siku ya Alhamisi, na kuua watu wawili na kuteka nyara 40 wengine, Anayeyi amesema.

The post Watu watano wauawa na wanamgambo mashariki mwa DRC appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/jg7JeCL

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT