Skip to main content

Uchumi wa dunia unajikokota, IMF kusema

IMF limesema kwamba inatarajia viwango vya ukuaji kushuka kutoka asilimia 6.1 ilivyokuwa mwaka jana, hadi asilimia 3,2 mwaka huu, ikiwa idadi ya chini kuliko ilivyotabiriwa mwezi Aprili.

Ukuaji uliotarajiwa mwaka jana ulifuatiwa na hali ngumu mwaka huu pale masuala mengi yalipoanza kujitokeza. Uzalishaji wa bidhaa kote ulimwenguni ulishuka kwenye robo ya kwanza ya mwaka huu kutokana na hali huko China na Russia ,wakati pia matumizi ya wanunuzi Marekani yalishuka kuliko ilivyotarajiwa.

IMF yenye makao yake Washington imesema kwamba uchumi wa dunia umepitia misukosuko kadhaa wakati ambapo ulikuwa tayari umepigwa vibaya na athari za janga la corona. Kuna hali ya kushuka kwa thamani ya fedha kote ulimwenguni na hasa hapa Marekani na kwenye mataifa ya Ulaya, hali iliyopelekea masharti magumu ya kiuchumi.

Uchumi wa China pia ulipungua kasi kuliko ilivyotarajiwa kutokana na janga la corona, lililopelekea kufungwa kwa shughuli za kawaida na hatimaye uvamizi wa Russia nchini Ukraine. IMF imesema kwamba bei za bidhaa muhimu kama chakula na mafuta zimeendelea kupanda kote ulimwenguni. Gharama ya maisha inakisiwa kupanda kwa asilimia 6.6 kwenye mataifa yaliyoendelea wakati asilimia 9.5 ikitarajiwa kwenye mataifa yanayoendelea.

The post Uchumi wa dunia unajikokota, IMF kusema appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/NrsSZaI

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT