Skip to main content

TIRA: Tunaunga mkono vijana kujiajiri

Na Hadia Khamis, Mtanzania Digital

MAMLAKA ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) imesema inaunga mkono juhudi zinazofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuondoa kiwango cha akiba maalumu (fixed deposit)ili vijana waweze kujiajiri zaidi.

Imesema kiwango hicho kimekuwa ni changamoto kubwa kwa watoa huduma za bima kwa sababu gharama yake ni kubwa.

Akizungumza na Mtanzania Digital leo katika maonyesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (DITF), Meneja wa TIRA, Frank Fred amesema lengo la kutoa kiwango hiko ni kutaka kuona sekta ya bima inakua zaidi na watu kutoa huduma kwa watu wengi na iliyo bora.

Fred amesema ghalama ya kujiunga kuwa wakala wa bima ilikuwa ni sh.milioni 1.8 wameiondoa baada ya kusikiliza ushauri wa Serikali ikiwemo wadau wa sekta hiyo.

“Tunatekeleza agizo la Rais na tinamuunga mkono kwa juhudi anazozifanya katika kuendeleza ajira za vijana,” amesema Fred.

Ameongeza kuwa Al hivi sasa wana makampuni wa wakala zaidi ya 32 ambapo kila kampuni kama itatoa ajira 100 kwa vijana kunakuwa na ajira 302 ambapo itapunguza tatizo la ajira .

Pia katika katika maonyesho hayo ya 46 wamekuja kuwafahamisha wadau wa sekta ya bima kuwa wameanzisha muongozo kwa makampuni ya simu kuweza kuingia ubia kwa wadau wa bima kwa kutumia simu za mkononi .

Aidha, kupitia maonyesho hayo TIRA itatoa mafunzo kwa wadau wao ambao watakaopita katika banda lao kuhusu muongozo wa bima ya takafu ambayo itakayowawezesha watu wa dini zote kitumia muongozo huo.

“Watu wengi wanadhani huu muongozo wa bima ya takafu upo kwa ajili ya waislamu lakini si kweli watu wote wanatakiwa kutumia bima hiyo,” amesema.

The post TIRA: Tunaunga mkono vijana kujiajiri appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/31032/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT