Skip to main content

“TCRA jengeni banda la kudumu Sabasaba”-Nnauye

*Atoa neno kwa TTCL

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye ameiagiza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kujenga jengo la kudumu ndani ya viwanja vya maonyesho ya Kimataifa ya Biashara (DITF) ili wananchi waweze kupata huduma iliyo bora.

Akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kufanya ziara ya kutembelea mabanda mbalimbali amesema ameshaongea na Mamlaka ya Biashara Tanzania (TANTRADE) juu ya TCRA kuwa na ofisi ya kudumu ndani ya uwanja kwa kuwa wanamajukumu makubwa kwa jamii.

Nnauye amesema uwepo wa banda la kudumu la TCRA ndani ya maonyesho hayo litarahisha wananchi kupata huduma kwa wakati, kupunguza gharama ambazo zinatumiwa na mamlaka hiyo kila mwaka wakati wa maonyesho..

“TCRA ni wadau muhimu kwa Watanzania kama mtakuwa na jengo lakudumu mtaweza kuwasaidia walio wengi kuweza kupata huduma sahihi,” amesema Nnauye.

Ameongeza kuwa Tanzania ni sehemu sahihi ya uwekezaji hivyo mawasiliano yakipatikana katika ubora itaongeza ubora zaidi.

Aidha, amesema licha ya makampuni ya nje kuwekeze Tanzania, TCRA isisite kutoa huduma kwa Watanzania .

“Pamoja na huduma zote mnazotoa Mtanzania anatakiwa apewe kipaumbele katika suala zima la utoaji huduma,” amesema Waziri Nnauye.

Ameongeza kuwa ni jukumu la vyombo vya habari kutangaza vitu vizuri vilivyopo Tanzania ili kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan.

Katika hatua nyingine Waziri Nnauye aametembelea banda la Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) na kuzitaka taasisi za Serikali kutumia teknolojia ya TEHAMA ya video Conference katika mikutano yao.

Amesema TEHAMA itasaidia kupunguza gharama kwa serikali na itawawezesha kuwasiliana kwa urahisi zaidi kwa watumishi wao.

“Serikali ipo tayari kuwawezesha kutekeleza mpango huo wa TEHAMA,” amesema Nnauye.

Nae Mkurugenzi wa TTCL, Mhandisi Peter Ulanga amesema wao ndio wa kwanza kutekeleza agizo la serikali la kutumia video conference katika mikutano, huku wateja wengi wakiwa jijini Dodoma.

The post “TCRA jengeni banda la kudumu Sabasaba”-Nnauye appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/du5Uith

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT