Skip to main content

SALAH AJIFUNGA LIVERPOOL


MSHAMBULIAJI wa Klabu ya Liverpool na Timu ya Taifa ya Misri Mohamed Salah ameongeza mkataba mpya wa miaka mitatu wa kuendelea kubakia katika klabu hiyo yenye maskani yake mitaa ya mersesyde.

Salah amesaini mkataba huo unaotarajiwa kumalizika majira ya kiangazi mwaka 2025 huku akipokea kitita cha Paundi 350,000 ambayo ni sawa na zaidi ya Milioni 982 kwa wiki za kitanzania

Kwa mkataba huo mpya Salah anaweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kupokea mshahara mkubwa katika historia ya klabu hiyo.

“Najisikia furaha na natarajia kuchukua makombe na klabu hii, ni siku nzuri kwa kila mtu.” Alisema Salah

“Inachukua muda kidogo kuongeza mkataba lakini kwa sasa kila kitu kipo sawa inabidi tufikirie yajayo, nadhani mnaweza kuona kwa kipindi cha miaka mitano ahdi sita timu imekuwa ikifanya vizuri. Msimu uliopita ilibaki kidogo tu tuchukue makombe manne lakini ndani ya wiki ya mwisho tukapoteza makombe mawili.

“Nadhani tupo katika nafasi ya kupambana kwa kila kitu. Tuna usajili mpya pia. Tunachotakiwa ni kuendelea kufanya kazi kwa bidii tuna maono mazuri na tupambanie kila kitu tena.”

Salah alijiunga na Liverpoo mwaka 2017 akitokea katika klabu ya AS Roma ambapo alifanikiwa kufunga jumla ya mabao 44 katika msimu wake wa kwanza kwa sasa ana umri wa miaka 30.

The post SALAH AJIFUNGA LIVERPOOL appeared first on Saleh Jembe.

The post SALAH AJIFUNGA LIVERPOOL appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/rTZYsL3

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT