Skip to main content

Rais Samia ataka mikakati uzalishaji wa chakula EAC

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

RAIS Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema Jumuiya ya Afrika Mashariki ina uwezo wa kuzalisha chakula kingi mara mbili ya kinachozaliwa sasa, iwapo kutakuwa na mikakati madhubuti.

Akizungumza katika mkutano wa 22 wa wakuu wa nchi saba za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ulioanza leo Julai 21, 2022 jijini Arusha, Rais Samia amesema EAC ina ardhi kubwa na ina uwezo wa kuzalisha chakula zaidi kuliko kinachozalishwa sasa.

Nafikiri tuangalie namna tunavyoitumia hiyo ardhi katika kuzalisha. Ardhi pekee haiwezi kufanikisha hilo, lazima tuangalie maji kupitia kilimo cha umwagiliaji je tutavunaje maji ya mvua. Hatuvuni maji ya mvua,” amesema Rais Samia.

Amesema ni lazima kuwe na skimu za umwagiliaji zitakazowezesha kilimo badala ya kutegemea mvua na kwamba, ili kuzalisha zaidi ni lazima jumuiya hiyo iangalie uwekezaji katika kilimo na kuwawezesha wakulima kuzalisha zaidi kupitia kilimo cha kisasa.

The post Rais Samia ataka mikakati uzalishaji wa chakula EAC appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/XuStF74

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT