Skip to main content

PSSSF yawataka wanachama wake kujisajili kidigital Sabasaba

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

MFUKO wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma, (PSSSF), umewataka wanachama wake kutembelea katika banda lao lililopo katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya 46 yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Julias Nyerere ili kuhakikiwa taarifa zao kwa mfumo wa alama za vidole.

Akizungumza na waandishi wa habari katika maonesho hayo, Meneja uhusiano wa PSSSF, James Mlowe amesema lengo la kuanzisha mfumo huo ni kupunguza mludikano wa Wanachama wao ambao wamekuwa wakifika katika ofisi zao.

Alisema kisheria kila mwaka wamekuwa wakifanya zoezi la kuhakiki Wana achama wao kwa njia ya kawaida.

“Kwa sasa tumeanzisha mfumo wa alama za vidole ambao umelenga kumsaidia mwanachama kutunza kumbukumbu zake vizuri na pia ataweza kutumia mfumo huu popote pale alipo,” amesema Mlowe.

Amesema huduma hiyo ya PSSSF kiganjani na PSSSF mtandaoni huduma hizo ni suluhisho la kuokoa muda kwa wanachama wastaafu pamoja na waajiri.

Mlowe amesema PSSSF imetenga Sh billioni 60 kwa wastafu zaidi ya160,000 ambazo uzitoa kwa kila mwezi kwa ajili ya kujikimu kiuchumi.

Aidha, amesema wanachama watakaotembelea banda lao watapata fursa ya kupata elimu kuhusu mfuko.

The post PSSSF yawataka wanachama wake kujisajili kidigital Sabasaba appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/31670/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT