Skip to main content

Polisi wa Uganda wawakamata waandamanaji wanaopinga kupanda kwa bei ya mafuta na chakula

Taifa hilo la Afrika mashariki lenye watu milioni 45 linakabiliwa na mdororo wa uchumi uliochochewa na janga la Covid 19, na hali hiyo ikazidi kuwa mbaya zaidi kutokana na vita vya Russia nchini Ukraine.

Mfumuko wa bei ya chakula uliongezeka maradufu hadi asilimia 13.1 mwezi Mei, kulingana na takwimu za hivi karibuni za serikali.

Jumatatu, waandamanaji walichoma matairi na kufunga barabara kuu yenye shughuli nyingi huko Jinja, umbali wa kilomita 80 mashariki mwa mji mkuu Kampala, wakiomba serikali kutoa ruzuku ya chakula kinachotumiwa sana.

“Polisi walitumia nguvu za wastani ikiwemo gesi ya kutoa machozi kutawanya waandamanaji, “ msemaji wa polisi katika eneo hilo James Mubi ameiambia AFP.

“Wanane kati ya viongozi wa maandamano hayo wamekamatwa,” amesema, akiongeza kuwa watashtakiwa leo Jumanne kwa kuchochea vurugu.

Waandamanaji walilazimisha waendesha magari kujiunga nao ili kuomba mabadiliko, mashahidi wameiambia AFP.

Bei ya mafuta, chakula na bidhaa msingi zimeongezeka sana ulimwenguni kwa sababu ya vita vya Ukraine, na kuathiri nchi maskini barani Afrika na kwingineko.

Nchini Uganda, lita moja ya petroli inauzwa shilingi 7,000, sawa na dola 1.85, ikiwa imeongezeka mara mbili tangu mwezi Februari. Katika baadhi ya maeneo ya mbali nchini humo, vituo vya mafuta vinauza lita moja hadi shilingi 10,000.

The post Polisi wa Uganda wawakamata waandamanaji wanaopinga kupanda kwa bei ya mafuta na chakula appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/34160/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT