Skip to main content

Picha| PSPTB yawakaribisha Wananchi kutembelea banda lake Sabasaba

Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Dk. Alban Mchopa, akikabidhiwa zawadi na Meneja Masoko na Uhusiano wa Bodi hiyo, Shamim Mdee(wapili kulia) baada ya kupata maelezo ya huduma zinazoendelea kwenye banda hilo Julai 6, 2022 kwenye maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam(SABASABA). wengine wanaoshuhudia ni watumishi wa bodi hiyo.

Picha ya pamoja ya Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Godfred Mbanyi(wa kwanza kulia) akiwa pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi, Charles Mnyeti(watatu kutoka kulia) na Dk. Alban Mchopa(watatu kutoka kushoto) wakiwa na watumishi wa PSPTB kwa ajili ya maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA).

Banda la Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) lipo ndani ya jengo la Wizara ya Fedha na Mipango ambapo pia inatoa huduma ya kuhuisha taarifa, elimu ya jinsi ya kujisajili kwa ajili ya Mitihani ya PSPTB na Uanachama kwa njia ya mtandao.

Hivyo, Bodi hiyo imewahimiza Watanzania mbalimbali kutembelea banda hilo kwa ajili ya kupata taarifa mbalimbali zinazohusiana na fani hiyo.

The post Picha| PSPTB yawakaribisha Wananchi kutembelea banda lake Sabasaba appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/du5Uith

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT