Skip to main content

Mwanahabari wa Marekani azuiliwa Congo

Kwa mujibu wa shirika la habari la AFP, asasi za kiraia kama vile RECN zimekaririwa na vyombo vya habari vya zikisema kwamba Niarchos pamoja na mwandishi wa habari wa Congo walikamatwa Jumatano katika mji wa kusini mashariki wa Lubumbashi, na kisha kupelekwa mji mkuu wa Kinshasa.

Afisa wa ngazi juu wa sserikali ambaye hakutaka kutajwa jina lake ameithibitisha AFP Jumapili kwamba Niarchos anashikiliwa na idara ya kijasusi ya ANR mjini Kinshasa. Afisa huyo ameongeza kusema kwamba Niarchos mwenye umri wa miaka 33, na ambaye huandikia magazeti ya Marekani ya The Nation na The New Yorker, amekuwa akiwasiliana na makundi yenye silaha likiwemo kundi la Bakata Katanga.

Mwaka 2017, wataalam wawili kutoka Marekani na Sweden waliokuwa wametumwa na Umoja wa mataifa kuchunguza ghasia kwenye eneo la Kasai nchini humo walitekwa nyara na kisha kuuwawa na watu wasiojulikana.

The post Mwanahabari wa Marekani azuiliwa Congo appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/36442/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT