Skip to main content

Mwakilishi wastaafu VETA aitaka jamii kuiamini mamlaka hiyo

Na Hadia Khamis, Wetu, Mtanzania Digital

Mwakilishi wa Wastaafu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Stephen Lazaro ameitaka jamii kuendelea kuiamini mamlaka hiyo kwani inauwezo mkubwa wa kutoa wanafunzi waliobobea katika fani mbalimbali.

Akizungumza wakati alipotembelea katika banda hilo liliopo katika maonyesho ya 46 ya Kimataifa ya Biashara maarufu Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam, Lazaro amesema Veta imeendelea kuboresha na kubuni vitu mbali mbali siku hadi siku.

“Jamii iendelee kuiamini Veta kwa kushirikiana nao lakini pia kwa kuleta wanafunzi ili kuweza kupata mafunzo yenye ubora yatakayoweza kuwasaidia kuweza kujiajiri wenyewe.

“Sisi ni wastaafu wa miaka mitano iliyopita lengo hasa la kutembelea Veta ni kwa sababu tumeitumikia lakini tumefurahi kuona jitihada za ubunifu zilizofanywa na wanafunzi pamoja na walimu wao,” amesema Lazaro.

Ameongeza kuwa kwasasa Veta inatumia teknolojia inayotumika viwandani ili kutoa wanafunzi waliobobea kwenye mafunzo ya viwanda.

The post Mwakilishi wastaafu VETA aitaka jamii kuiamini mamlaka hiyo appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/32413/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT