
AIU, inayosimamia masuala ya uadilifu katika riadha ya kimataifa ikiwa ni pamoja na utumiaji wa dawa za kuongeza nguvu, imesema vipimo vilivyofanyiwa Cherono vimegundua kwamba ametumia dawa ya aina ya trimetazidine.
Hiyo ni moja kati ya dawa zilizoko kwenye orodha ya Idara ya kupambana na dawa za kuongeza nguvu zilizopigwa marufuku kwa mwaka 2022.
Cherono mshindi wa mbio za marathon za Boston na Chicago mwaka 2019, alitoa sampuli ya damu na mkojo wake kabla ya mashindano hapo May 23 na kuarifiwa matokeo alipofika Eugene siku ya Alhamisi.
Kwa upande wa Ross, taarifa ya AIU ina sema mwanariadha huyo aliyeshiriki katika timu ya mbiyo za mita 400 kupokezana iliyoshinda nishani ya dhahabu mwaka jana kwenye mashindano ya Olympiki amesitishwa kutokana na tabia yake wakati wa uchunguzi kuweza kufahamu mahala alikuwepo.
Mashindano yote ya awali ya Marathon na mita 400 yanafanyika Jumapili kwa hivyo hawatoweza kushiriki.

The post Mkenya Cherono na Marekani Ross wasitishwa mashindano mabingwa wa riadha duniani appeared first on soka letu.
Via soka letu https://ift.tt/lXB9LOg
Comments
Post a Comment