Skip to main content

Mapigano ya risasi kati ya magenge hasimu huko Haiti yamesababisha vifo vya watu 50

Mapigano ya risasi kati ya magenge hasimu yamesababisha vifo vya watu 50 tangu Ijumaa karibu na mji mkuu wa Haiti wa Port-au-Prince, Meya wa eneo hilo alisema Jumatatu huku ghasia zikiendelea kusambaa katika taifa hilo la Caribbean.

Mapigano ya risasi kati ya magenge kwenye kitongoji maskini cha Cite Soleil, pia yamesababisha zaidi ya watu 100 kujeruhiwa, kulingana na Meya wa Cite Soleil, Joel Janeus, akiongeza kwamba 50 kati ya hao wako katika hali mbaya.

Magenge hayo pia yamezuia ufikiaji wa kituo cha mafuta cha Varreux gazeti la Haiti Le Nouvelliste liliripoti. West Indies Group, kundi la Haiti ambalo linamiliki uwanja wa Varreux halikujibu mara moja ombi la kutoa maoni yao.

Ofisi ya waziri mkuu, Ariel Henry, haikujibu mara moja ombi la maoni hayo. Ghasia hizo zinaonekana kuwa matokeo ya makabiliano kati ya G9 na magenge ya GPEP.

Ghasia za magenge zimeongezeka tangu Rais Jovenel Moise, alipouawa mwaka mmoja uliopita katika uvamizi uliofanyika usiku, na kusababisha vuguvugu la kisiasa na makundi ya uhalifu kupanua udhibiti wao katika eneo la nchi hiyo.

Wanaharakati wa haki mwezi Mei walisema mapigano kati ya mpinzani Chen Mechan na magenge 400 ya Mawozo yamesababisha vifo vya watu 148, baadhi yao walikufa kwa kukatwakatwa kwa mapanga au walifariki wakati nyumba zao zilipochomwa moto.

The post Mapigano ya risasi kati ya magenge hasimu huko Haiti yamesababisha vifo vya watu 50 appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/PaYHjz0

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT