Skip to main content

Makombora ya Russia yaua watu 22 katika mji wa Ukraine wa Vinnytsia

Polisi wamesema jengo la ofisi katikati mwa mji huo, lililoko umbali wa kilomita 270 kusini magharibi mwa mji mkuu, Kyiv, lilishambuliwa na makombora matatu.

Makombora hayo ambayo yalirushwa kutoka manwari ya Russia katika bahari nyeusi, yaliharibu majengo ya makazi katika eneo hilo na kuteketeza magari 50 yaliyokuwa yameegeshwa karibu na eneo hilo.

Gavana wa jimbo la Vinnytsia, Serhiy Borzov, amesema vifaa vya ulinzi wa anga ya Ukraine vilidungua makombora mengine manne juu ya eneo hilo.

Vinnytsia ni mmoja ya miji mikubwa ya Ukraine, ukiwa na wakazi 370,000. Maelfu ya watu kutoka mashariki mwa Ukraine, ambako Russia imejikita zaidi katika mashambulizi yake, walikimbilia kwenye mji huo wa Vinnytsia tangu kuanza kwa vita tarehe 24 Februari.

Umoja wa mataifa umesema watoto watatu ni miongoni mwa waliouawa katika shambulio la Vinnytsia.

The post Makombora ya Russia yaua watu 22 katika mji wa Ukraine wa Vinnytsia appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/35292/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT