Skip to main content

Jumuiya ya kiraia Sudan imekataa pendekezo la Mkuu wa jeshi nchini humo la serikali ya kiraia

Jumuiya kuu ya kiraia nchini Sudan siku ya Jumanne ilikataa pendekezo la kiongozi wa mapinduzi ya nchi hiyo la kutoa nafasi kwa serikali ya kiraia kama njia ya ujanja na kuhimiza maandamano zaidi.

Mkuu wa jeshi Abdel Fattah al-Burhan ambaye unyakuzi wake wa madaraka hapo Oktoba mwaka 2021 ulizuia mpito kwa utawala wa kiraia aliapa kwa mshangao Jumatatu kutoa nafasi kwa makundi ya kiraia kuunda serikali mpya ya mpito.

Lakini muungano mkuu wa kiraia The Forces for Freedom Change (FFC) ulitoa wito wa kuendeleza shinikizo la umma mitaani na kutupilia mbali hatua ya Burhan na kusema ni mbinu ya ujanja wa uwazi. Hotuba ya kiongozi wa mapinduzi ni hila kubwa na mbaya zaidi kuliko mapinduzi ya Oktoa 25 kiongozi wa FFC, Taha Othman alisema.

Mgogoro huo utaisha kwa viongozi wa mapinduzi kujiuzulu na vikosi vya mapinduzi kuunda serikali ya kiraia. Maandamano pia yalienea katika miji mingine Jumanne ikiwa ni pamoja na Wad Madani uliopo kilomita 200 kusini mwa mji mkuu ambapo mamia ya waandamanaji walifanya maandamano ya kukaa chini kulingana na mashahidi.

The post Jumuiya ya kiraia Sudan imekataa pendekezo la Mkuu wa jeshi nchini humo la serikali ya kiraia appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/32041/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT