Skip to main content

IMF imekubali kufufua mpango wa kuisaidia kufedha Pakistan

Shirika la fedha la kimataifa (IMF) limekubali kufufua mpango wa kuisaidia kifedha Pakistan na kutoa unafuu wakati ambapo bei kubwa ya kimataifa ya uagizaji wa nishati inaisukuma nchi hiyo kwenye uhaba wa pesa huku ikikumbwa na tatizo la malipo.

Taarifa ya IMF ya Jumatano jioni ilisema wafanyakazi wake na maafisa wa Pakistan wamefikia makubaliano kuhusu sera zinazo fanyiwa tathmini za mpango wa ufadhili wa kimataifa wa taasisi ya upanuzi (EFF) kwa Islamabad. Makubaliano yaliyofikiwa na wafanyakazi ikiwa yataidhinishwa na bodi ya IMF yataleta jumla ya malipo chini ya mpango huo hadi karibu dola bilioni 4.2

Waziri wa fedha wa Pakistan, Miftah Ismail alisema katika Twitter kwamba Pakistan hivi karibuni itapokea awamu ya kwanza ya dola bilioni 1.17.

Pakistan iko katika wakati mgumu wa kiuchumi. Mazingira magumu ya nje pamoja na sera za ndani vilichochea mahitaji ya ndani hadi kufikia viwango visivyoweza kudumu, alisema Nathan Porter, ambaye aliongoza timu ya IMF katika wiki za mazungumzo na Islamabad.

Taarifa ya IMF ilibainisha kuwa bodi yake pia itazingatia kurefusha program ya EFF hadi mwisho wa Juni mwaka 2023 na iwapo itaongeza karibu dola bilioni moja. akiba ya fedha za kigeni katika benki kuu imeshuka hadi karibu dola bilioni 9.7 ambazo hazitoshi kugharamia wiki chache za uagizaji bidhaa kutoka nje. Rupia pia ilishuka hadi chini ya historia dhidi ya dola ya Marekani katika wiki za hivi karibuni.

The post IMF imekubali kufufua mpango wa kuisaidia kufedha Pakistan appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/35294/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT