Skip to main content

Ethiopia yasema ipo tayari kwa mazungumzo na TPLF bila masharti

Kwa mujibu wa shirika la habari la AP, matamshi hayo yametolewa na Redwan Hussein mshauri wa usalama wa waziri mkuu Abiy Ahmed, wakati kukiwa na matumiani ya kuwepo majadiliano ya kusuluhisha mapigano yaliyozuka hapo Novemba 2020.

Redwan alitweet baada ya mkutano na wawakilishi maalum kutoka Umoja wa mataifa , Umoja wa Ulaya na Marekani, akiongezea kwamba Umoja wa Afrika utaongoza mchakato huo, na kwamba unaweza kuomba msaada wa kiufundi kutoka kokote.

Baada ya sitisho la mapigano la Juni, pamoja na kuruhusiwa upelekaji wa misaada kwenye eneo la Tigray, pande zote mbili zilikubaliana kufanya mazungumzo. Serikali kuu ya Ethiopia iliteua wapatanishi 7 wakiongozwa na waziri wa mambo ya nje ingawa upande wa Tigray unasema ni lazima masharti kadhaa yatimizwe kabla ya mazungumzo hayo kufanyika.

Mapema wiki hii, kiongozi wa serikali ya kieneo ya Tigray Debretsion Gebremichael alisema kwamba iwapo serikali kuu ina azma ya kweli ya kurejesha amani, basi ingeanza kwa kurejesha huduma za msingi katika mkoa huo kama vile umeme, mawasiliano ya simu na benki.

Wakosoaji wanasema kwamba hatua inayohitajika ni kuondolewa kwa viongozi wa Tigary pamoja na kupokonywa silaha kwa wapiganaji wao, kabla ya mazungumzo kuanza. Baadhi wanasema pia kwamba itakuwa kinyume cha sheria kwa serikali kufanya mashauriano na TPLF wakati bado liko kwenye orodha ya serikali ya Ethiopia ya makundi ya kigaidi.

Serikali ya Ethiopia imekuwa katika shinikizo la kimataifa kufanya mashauriano na viongozi wa Tigray, ili kumaliza mapigano ambayo yameua maelfu ya watu kwenye eneo hilo pamoja na mikoa jirani ya Amhara na Afar.

The post Ethiopia yasema ipo tayari kwa mazungumzo na TPLF bila masharti appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/40970/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT