Skip to main content

Chuo Kikuu Mzumbe chawakaribisha Wanafunzi na Wawekezaji kwenye banda lake Mnazi mmoja

Na Faraja Masinde, Mtanzania Digital

Chuo Kikuu cha Mzumbe kimewakaribisha wanafunzi wa wanaotaka kusoma fani mbalimbali mbalimbali kutembelea banda lake ili kujua programu mbalimbali zinatolewa na chuo hicho ikiwamo ushauri wa kitaalamu.

Dk. Faida Fundi wa Shule ya Utawala na Menejimenti ya Chuo Kikuu Mzumbe(kulia) akitoa maelekezo kwa mmoja wa wanafunzi aliotembelea banda la chuo hicho katika maonyesho ya Vyuo vya Elimu ya Juu yanayoendela katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Aidha, chuo hicho pia kimewakaribisha wawekezaji wanaotka kuwekeza kwenye chuo hicho kutembelea banda hilo kwa ajili ya kufahamu sera yake ya uwekezaji.

Hayo yamebainishwa Julai 18, 2022 na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko wa chuo hicho, Rose Joseph wakati akizungumza na Mtanzania Digital katika maonyesho ya Vyuo Vikuu yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam yakihusisha vyuo mbalimbali.

Rosema amesema chuo hicho kina zaidi ya programu 44 kuanzia ngazi ya Stashahada hadi Shahada ya Uzamivu(PhD) ambapo mwanafunzi akifika kwenye banda lao atapatiwa msaada wa kitaalamu juu ya fani anayotaka kusoma.

“Chuo Kikuu Mzumbe tunashikiriki katika haya maonyesho ya Vyuo Vikuu ambayo yameandaliwa na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania(TCU), na kikubwa tunachokifanya hapa ni kuweza kuwafamisha wanafunzi na Watanzania kwa ujumla juu ya programu zetu zaidi ya 44 ambazo tunatoa kuanzia ngazi ya Stashahada hadi Shahada ya Uzamivu.

“Hivyo mwananchi ambayo anataka kujua zaidi juu ya programu hizi tunazozitoa tunamkaribisha Mnazi Mmoja ndani ya banda letu kwa ajili ya kupata mwongozo kutoka kwa wataalamu wetu kwani pia tunatoa ushauri wa kitaalamu bure kulingana na ufaulu wa mwanafunzi na ni fani zipi ambazo anaweza kuomba ndani ya chuo chetu,” amesema Rose.

Rose amewahimiza wahitimu wa kidato cha nne, cha sita na kuendelea kwa ajili ya kufika kwenye banda hilo ili kujua ni kwa namna gani ya kujiendeleza huku akiwahimiza pia wawekezaji.

“Mbali na wanafunzi, pia tunawakaribisha wahitimu wa degrii kufika kwenye banda letu kwani elimu haina mwisho na kuona ni kwa namna gani wanaweza kujiendeleza.

“Pia hii ni fursa kwa wadau wetu waliosoma katika chuo chetu cha Mzumbe kufika kwa ajili ya kuona mambo mbalimbali yanayotekelezwa na chuo na kuona ni kwa namna gani nao wanaweza kutoa mchango wao katika kuboresha chuo chetu.

“Sambamba na hilo tunawakaribisha wawekezaji katika sekta mbalimbali kufika kwenye banda letu ili kujifunza sera ya uwekezaji na kuona ni namna gani wanaweza kushirkiana na chuo kwenye sekta hiyo, hivyo tunawakaribisha waje ili tuweze kujadiliana,” amesema Rose.

Maonyesho hayo ya Vyuo Vikuu ambayo yameanza Jumatatu ya Julai 18, yanatarajiwa kuhitimishwa Julai 22, mwaka huu.

The post Chuo Kikuu Mzumbe chawakaribisha Wanafunzi na Wawekezaji kwenye banda lake Mnazi mmoja appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/GgTh7pa

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT