Skip to main content

Balozi Dk. Bana, maofisa watembelea miradi ya Dangote Nigeria

Na Mwandishi Maalum, Nigeria

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Nigeria, Dk. Benson Bana na maofisa wa Ubalozi wametembelea mji wa viwanda wa Kampuni ya Dangote (Dangote industrial city) katika jiji la Lagos nchini hapa.

Mji huo unajumuisha ujenzi wa mitambo mikubwa ya kisasa ya kusafisha mafuta ghafi, kiwanda cha mbolea, kiwanda cha kuzalisha plastiki (petro-chemical) na bandari binafsi ya meli za mizigo ambapo mmiliki wake ni mfanyabiashara na tajiri namba moja barani Afrika, Alhaji Aliko Dangote, raia wa Nigeria.

Tajiri huyo amewekeza nchini Tanzania kwa kujenga kiwanda cha kuzalisha saruji katika mkoani Mtwara, ambapo pamoja na mambo mengine, ziara hiyo ilikusudia kuendeleza uhusiano mwema kati ya Tanzania na kampuni ya Dangote, pamoja na hilo Balozi Bana aliishukuru kampuni hiyo kwa kuwekeza nchini Tanzania na aliusihi na kushawishi uongozi wa Dangote kuona uwezekano wa kuongeza uwekezaji wake nchini Tanzania hususani Ujenzi wa Kiwanda cha Mbolea kutokana na uwepo wa gesi ya kutosha.

Aidha, alimpongeza Mwenyekiti wa Kampuni za Dangote, Alhaji Aliko Dangote kwa kufanya ziara nchini Tanzania, Mei 24, mwaka jana ambapo alikutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Alimpongeza kwa ahadi yake kuwa popote atakapokwenda duniani atawashawishi wafanyabiashara wenye mitaji kuwekeza Tanzania kutokana na maboresho anayoyafanya Rais Samia Suluhu Hassan katika mawanda ya uwekezaji na biashara.

Aidha, Balozi alimsihi Alhaji Dangote kutekeleza nia yake ya kuwekeza katika uzalishaji mbolea nchini Tanzania.

“Hatua zinazochukuliwa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika kuboresha mazingira ya kufanya biashara Tanzania ili kuwavutia wawekezaji na mitaji zinakwenda kuleta mageuzi ya kweli na mazingira salama kwa wekezaji katika nchi yetu,” amesema Balozi Dk. Bana

Kwa upande wa Uongozi wa kampuni ya Dangote, ulimweleza Balozi kuwa nia ya kujenga kiwanda cha mbolea nchini Tanzania bado ipo na kwamba kampuni hiyo itaendelea kupanua miradi yake katika nchi mbalimbali barani Afrika, ikiwemo Tanzania.

Ilielezwa kuwa, hatua za awali hasa utafiti wa ujenzi wa bandari (jet) kwa ajili ya uwekezaji huo, zilishafanyika na mpango wa kuutekeleza unaendelea.

Pamoja na hilokampuni hiyo imekamilisha ufungaji wa mitambo ya kusafisha mafuta na iko katika hatua za mwisho kukamilisha uhakiki wa mitambo ya kusafisha mafuta. Lengo ni kuanza usafishaji mafuta mwishoni mwa mwaka 2022. Kiasi cha cha pipa za mafuta gafi 650,000 sawa na lita 102,700,000 zitasafishwa kwa siku.

Mafuta yatakayokuwa yanazalishwa yatakuwa kwa ajili ya soko la ndani na nje ya Nigeria. Uwekezaji katika mradi huo wa kusafisha mafuta wenye jumla ya miradi 19, unatarajia kuwa wa thamani ya Dola za Marekani zaidi ya bilioni 20. Idadi ya wafanyakazi 20,000 hadi 50,000 waliajiriwa katika hatua mbalimbali za ujenzi.

The post Balozi Dk. Bana, maofisa watembelea miradi ya Dangote Nigeria appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/31329/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT