Skip to main content

Afrika Kusini: Polisi wawakamata watu wawili kuhusiana na shambulizi kwenye kilabu cha pombe

Kukamatwa kwa watu hao kumetokea kufuatia uchunguzi kuhusu shambulizi la bunduki la Jumamosi usiku kwenye kilabu cha pombe katika mji wa mashariki wa Pietermaritzburg katika jimbo la KwaZulu Natal, ambako watu wanne waliuawa na wengine wanane kujeruhiwa wakati wanaume wawili walipowafyatulia risasi kiholela wateja.

Wizara ya polisi imeeleza katika taarifa kukamatwa kwa watu hao kama hatua ya kwanza ya kuwaweka kizuizini wale wote waliopanga moja ya mauaji mabaya zaidi nchini mwishoni mwa juma.

Watu wengine 15 wakiwemo wanawake wawili, waliuawa kwa kupigwa risasi mapema Jumapili wakati wakiburudika usiku katika kitongoji cha Soweto, karibu na Johannesburg, katika tukio tofauti.

Mashambulizi ya bunduki ni jambo la kawaida nchini Afrika Kusini, ambayo ina moja ya viwango vya juu vya mauaji duniani, yanayochochewa na vurugu za magenge yenye silaha na ulevi wa pombe.

The post Afrika Kusini: Polisi wawakamata watu wawili kuhusiana na shambulizi kwenye kilabu cha pombe appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/34158/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT