Skip to main content

Wizara ya Elimu yaipatia NIT Bilioni 49 kuanzisha kituo cha umahiri

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia mradi wa EASTRIP imekipatia Chuo cha Usafirishaji (NIT) zaidi ya Sh bilioni 49 kwa ajili ya kukiwezesha Chuo hicho kuanzisha Kituo cha Umahiri cha Mafunzo ya Taaluma ya Usafiri wa Anga na Operesheni za Usafirishaji.

Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam na Naibu Katibu Mkuu, Prof. Carolyne Nombo wakati akizindua vifaa vya mafunzo ya uhandisi na matengenezo ya ndege vilivyonunuliwa na mradi huo.

Amesema fedha hizo ni mkopo kutoka Benki ya Dunia zimetolewa kwa chuo hicho kwa kutambua mchango wake katika kuandaa wataalamu wenye weledi na ujuzi katika fani za usafirishaji na uchukuzi.

Prof. Nombo amesema Serikali ya Awamu ya Sita imekuwa ikifanya kila linalowezekana ili kuhakikisha mafunzo yanayotolewa katika vyuo vyetu yanaakisi mahitaji ya sekta husika na hivyo kupata wahitimu wenye kuendana na mahitaji ya soko la ajira.

Akizungumzia vifaa maalum vilivyozinduliwa kwa ajili ya uhandisi wa matengenezo ya ndege amesema Serikali imetumia kiasi cha Sh bilioni 2.1 kwa ajili ya kukiongezea chuo uwezo wa kutoa elimu bora kwenye taaluma ya uhandisi wa matengenezo ya ndege.

“Lengo la Serikali ni kuhakikisha vyuo vya kimkakati kama hiki cha NIT, DIT na ATC vinatoa mafunzo yanayoakisi maendeleo ya nchi na yanayolenga kutatua changamoto zinazowakabili wananchi,” amesema Prof. Nombo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji, Mhandisi Prof. Blasius Nyichomba ameishukuru Serikali kwa kukiwezesha chuo hicho kupata vifaa vya kisasa vitakavyowezesha utoaji wa elimu katika Chuo hicho.

Naye Mkuu wa Chuo Mhandisi Prof. Zacharia Mganilwa ameeleza kuwa vifaa vilivyonunuliwa ni “runnable jet engine, motorized cutaway piston engine na virtual maintainance trainer” ikiwa ni moja ya mafaniko ya utekelezaji wa mradi huo.

Mmoja wa wanafunzi wa fani ya uhandisi matengenezo ya ndege wa chuo hicho, Makame Abdalla ambae amebuni mfumo wa uondoshaji barafu kwenye mabawa ya ndege ameishukuru Serikali kwa kukiwezesha chuo hicho kupata vifaa vya kujifunzia na ametoa rai kwa wanafunzi wanaotaka kusoma fani hiyo kusoma NIT kwa kuwa kina vifaa vya kutosha katika fani hiyo.

The post Wizara ya Elimu yaipatia NIT Bilioni 49 kuanzisha kituo cha umahiri appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/25436/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT