Skip to main content

Waziri mkuu wa Uingereza Johnson, anusurika katika kura ya kutokuwa na imani naye

Johnson ambaye alipata ushindi wa kishindo katika uchaguzi wa 2019, amekuwa chini ya shinikizo kubwa baada ya yeye na wafanyakazi wake kuanda sherehe ya kunywa pombe kwenye ofisi yake ya Downing street na nyumbani kwake wakati Uingereza ilikuwa chini ya masharti makali ya kukabiliana na janga la Covid 19.

Wabunge kadhaa wamesema, kuona wabunge 211 ndio walimuunga mkono na 148 wakapiga kura ya kumpinga, ni ishara mbaya kuliko ilivyokuwa inatarajiwa kwa waziri mkuu.

“Boris Johnson amepata afueni kwenye kura hii, lakini anatakiwa pia kuelewa kwamba kipaumbele cha kufuata ni kujenga umoja kwenye chama chake, David Jones, waziri mkuu wa zamani ameiambia Reuters.

Kwa kushinda kura ya kuwa na imani naye, Johnson amepata afueni kwa miezi 12 ambapo wabunge hawawezi kuleta changamoto nyingine.

Baada ya kura hiyo, Johnson amesema hana mpango wa kuitisha uchaguzi wa kitaifa wa haraka.

“Nadhani ni matokeo ya kuridhisha kwa siasa na nchi, ni matokeo madhubuti na maana yake ni kwamba kama serikali tunaweza kuendelea na kujikita kwenye mambo ambayo nadhani ni muhimu kwa wananchi,” amemwambia mwandishi wa habari.

The post Waziri mkuu wa Uingereza Johnson, anusurika katika kura ya kutokuwa na imani naye appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/21993/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT