Skip to main content

Watu watatu wauawa katika shambulio dhidi ya makanisa mawili Nigeria

Shambulio hilo katika eneo la Kajuru katika jimbo la Kaduna lililenga vijiji vinne, na kusababisha utekaji nyara wa wakazi ambao idadi yao haikuthibitishwa na uharibifu wa nyumba kabla ya washambuliaji kutoroka, wenyeji wamesema.

Haikufamika mara moja waliofanya shambulio hilo kwenye makanisa huko Kaduna.

Sehemu kubwa ya Nigeria imekuwa ikikumbwa na matatizo ya usalama, Kaduna ikiwa ni moja ya majimbo yaliyoathirika sana. Wiki iliyopita, watu 32 waliuawa katika eneo la Kajuru katika shambulio lililodumu saa kadhaa.

Waumini walikuwa wamehudhuria Jumapili asubuhi ibada ya misa kwenye kanisa la Kibaptist la Maranatha na kanisa la Katoliki la mtakatifu Moussa katika jamii ya Rubu ya Kaduna, wakati washambuliaji walifika eneo hilo na kuzingira makanisa hayo yote yakiwa katika eneo hilo, amesema Usman Danladi ambaye anaishi karibu na eneo hilo.

Serikali ya jimbo la Kaduna imethibitisha vifo vya watu 3 waliouawa na majambazi ambao walivamia vijiji wakiwa kwenye pikipiki.

Shirika la kikatoliki la Nigeria limelaani mashambulizi ya Jumapili na kusema kwamba makanisa nchini Nigeria yamekuwa yakilengwa na makundi yenye silaha.

The post Watu watatu wauawa katika shambulio dhidi ya makanisa mawili Nigeria appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/25892/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT