Skip to main content

Watu 6 wauawa katika mashambulizi ya ufyatuaji risasi katika miji tofauti ya Marekani

Washambuliaji wengi walifyatua risasi kwenye barabara ya Philadelphia ya South Street yenye shughuli nyingi, eneo lenye baa nyingi na migahawa, nyakati za saa sita usiku Jumamosi. Wanaume wawili na mwanamke mmoja waliuawa, maafisa wamesema.

“Kulikuwa na mamia ya watu wakifurahi kwenye barabara ya South Street, kama wanavyofanya kila mwishoni mwa juma, wakati ufyatuaji wa risasi ulipoanza,” mkuu wa polisi huko Philadelphia D.F. Pace amesema.

Katika tukio jingine, watu watatu waliuawa na wengine 14 kujeruhiwa baada ya shambulio la risasi karibu na baa moja katika mji wa Chattanooga, maafisa wamesema, wakiongeza kuwa watu wawili walifariki kutokana na majeraha ya risasi na mmoja alifariki kufuatia majeraha baada ya kugongwa na gari akikimbia kutoka kwenye eneo la tukio.

Waathirika watatu walijeruhiwa wakati wakijaribu kukimbia na waligongwa na magari, maafisa wa Tennessee wamesema, wakiongeza kuwa wengine kadhaa waliojeruhiwa wako katika hali mbaya.

Hapa Marekani mwaka huu, kumefanyika mashambulizi 240 yanayolenga watu wengi.

The post Watu 6 wauawa katika mashambulizi ya ufyatuaji risasi katika miji tofauti ya Marekani appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/21736/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT