Skip to main content

Wanajeshi wawili wauawa na waasi wa M23, jeshi la DRC lasema

Ni ghasia za hivi karibuni katika mzozo huo wa muda mrefu ambao uliibuwa katika wiki za hivi karibuni na kusababisha mvutano wa kidiplomasia na nchi jirani ya Rwanda.

Waasi wa M23 walishambulia kwa makombora kituo cha jeshi huko Kivu Kaskazini, na kuua wanajeshi wawili na kujeruhi wengine watano.

Congo inamshtumu jirani yake kuunga mkono kundi la M23, tuhuma ambazo Rwanda inakanusha.

Mapigano hayo yanafuatia uvamizi uliofanywa Jumapili kwenye kijiji cha mkoa jirani wa Ituri na wapiganaji wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa kiislamu kutoka kundi lingine la uasi na kuua watu 18, vyanzo vya eneo hilo vimesema.

Wapiganaji wanaoshukiwa kuwa wa kundi la Alliance Democratic Forces (ADF) waliua wakazi na kuchoma moto nyumba katika kijiji cha Otamabere, wamesema, shahidi mmoja, kiongozi mmoja na shirika la haki za binadamu katika eneo hilo.

Msemaji wa jeshi la Congo Jules Ngongo amethibitisha shambulizi la ADF bila kutoa idadi ya vifo.

The post Wanajeshi wawili wauawa na waasi wa M23, jeshi la DRC lasema appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/KStrdiz

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT