Skip to main content

Wacolombia wapiga kura kumchagua rais

Kura za maoni zinaonyesha mwanasiasa wa mrengo wa kushoto, Gustavo Petro, na mpinzani wake, Rodolfo Hernández – wote mameya wa zamani – wanana uungwaji mkono sawa, tangu kuwashinda wagombea wengine wanne katika uchaguzi wa awali wa tarehe 26 mwezi Mei ambapo hakuna aliyepata kura za kutosha kushinda moja kwa moja, na hivyo kulazimisha duru ya pili.

Takriban watu milioni 39 wanlitarajiwa kupiga kura loe Jumapili, lakini takwimu zinaonyesha kwamba, katika kila uchaguzi wa urais tangu mwaka wa 1990, zaidi ya asili mia 40 wamekuwa hawashiriki uchaguzi.

Raia wa Colombia wanapiga kura huku kukiwa na hali ya kutoridhika iliyoenea juu ya kuongezeka kwa ukosefu wa usawa, mfumuko wa bei na ghasia.

Wengi wameonyesha kutoridhika na hali ya nchi hivi kwamba katika duru ya kwanza waliwaondoa wanasiasa wa muda mrefu na wanaoegemea upande wa kulia, na kuchagua watu wawili ambao hawana historia ndefu ya siasa.

The post Wacolombia wapiga kura kumchagua rais appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/23cIPfd

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT