Skip to main content

Vikosi vya Russia vimeshambulia kiwanda cha kemikali kilichopo Ukraine

Vikosi vya Russia vilishambulia kwa mabomu kiwanda cha kemikali kinachohifadhi mamia ya wanajeshi na raia katika mji wa Sievierodonetsk huko mashariki mwa Ukraine siku ya Jumapili lakini gavana wa mkoa wa Luhansk alisema kiwanda hicho kiko chini ya udhibiti wa Ukraine.

Gavana Serhii Haidai alisema huo ni uongo unaotolewa na wanaotaka kujitenga wanaoungwa mkono na Russia kwamba wanajeshi 300 hadi 400 wa Ukraine wamekwama katika kiwanda cha Azot pamoja na mamia ya raia.

Eneo la kiwanda hicho linapigwa risasi Haidai alisema. Mapigano yanaendelea kwenye viunga vya jiji katika mitaa karibu na kiwanda hicho. Alisema moto mkubwa ulizuka kwenye kiwanda siku ya Jumamosi wakati wa shambulizi la Russia.

Russia inadai kwamba tayari inadhibiti asilimia 97 ya mkoa wa Luhansk. Lakini kuuteka mji wa viwanda wa Sievierodonetsk wenye wakaazi laki moja kabla ya vita bado ni muhimu kwa lengo pana la Moscow kudhibiti eneo la mashariki la Donbas ambalo linajumuisha mikoa ya Luhansk na Donetsk.

The post Vikosi vya Russia vimeshambulia kiwanda cha kemikali kilichopo Ukraine appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/23777/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT