Skip to main content

Uingereza imefuta safari ya ndege ya waomba hifadhi wahamiaji kurudishwa Rwanda

Uingereza imefuta safari ya ndege iliyokuwa imepangwa kuwapeleka waomba hifadhi nchini Rwanda siku ya Jumanne jioni baada ya mahakama ya ulaya ya haki za binadamu kuingilia kati ikisema mpango huo ulikuwa hatari ya kweli kwa madhara ambayo yasiyoweza kutenguliwa.

Uamuzi wa kufuta safari ya ndege ulitokana na siku tatu za changamoto kali za mahakama, kutoka kwa mawakili wa haki za wahamiaji ambao waliwasilisha msururu wa rufaa za kesi baada ya kesi wakitaka kuzuia kuondolewa kwa kila mtu aliyekuwa kwenye orodha hiyo ya serikali.

Maafisa wa serikali ya Uingereza walisema mapema Jumanne kwamba ndege hiyo ingeondoka bila kujali ni watu wangapi waliokuwemo ndani. Vyombo vya habari vya uingereza viliripoti kuwa idadi ya watu wanaotarajiwa kufukuzwa ilikuwa zaidi ya 30 siku ya Ijumaa.

Baada ya safari ya ndege kufutwa, waziri wa mambo ya ndani wa Uingereza Priti Patel alisema alisikitishwa lakini hatazuiliwa kufanya jambo sahihi. Aliongeza kuwa timu yetu ya sheria inakagua kila uamuzi uliofanywa kwenye safari hii ya ndege na maandalizi ya safari ya pili ya ndege yanaanza hivi sasa.

The post Uingereza imefuta safari ya ndege ya waomba hifadhi wahamiaji kurudishwa Rwanda appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/24426/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT