Skip to main content

Uganda na DRC zimeongeza muda wa shughuli za Operesheni Shujaa

Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) Jumatano ziliongeza operesheni ya pamoja ya kijeshi iliyoanzishwa mwishoni mwa mwaka jana dhidi ya waasi wa kiislam mashariki mwa Congo msemaji wa operesheni hiyo alisema.

Nchi ya Uganda ilituma takribani wanajeshi 1,700 kwa jirani yake wa Afrika ya kati hapo mwezi Disemba ili kusaidia kupambana na kundi la waasi lenye vurugu linalojulikana kama Allied Democratic Forces (ADF) uingiliaji mkubwa zaidi wa kigeni nchini Congo katika kipindi cha muongo mmoja kando na operesheni ya kulinda Amani ya Umoja wa mataifa.

Hapo awali ilikusudia kudumu kwa miezi sita. Operesheni Shujaa iliongezwa siku ya Jumatano licha ya tangazo la awali lililotolewa na jeshi la Uganda kwamba lingeondoa wanajeshi mara operesheni hiyo itakapokamilika kinyume na hapo kama itaelekezwa vinginevyo.

Msemaji wa Shujaa, Kanali Mak Hazukay aliliambia shirika la habari la reuters kuwa majeshi ya Congo na Uganda yalitia saini Juni mosi kuongeza muda wa operesheni zao za kijeshi katika awamu ya tatu, kwa sababu tishio hilo halijatokomezwa.

The post Uganda na DRC zimeongeza muda wa shughuli za Operesheni Shujaa appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/xr56wH4

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT