Skip to main content

Tume ya Umoja wa Ulaya imesema Croatia imetimiza vigezo vyote kujiunga na EU

Tume ya Umoja wa Ulaya ilisema Jumatano kwamba Croatia ilitimiza vigezo vyote vya kujiunga na ukanda wa ulaya na hivyo kufungua njia kwa nchi hiyo kuwa mwanachama wa 20 kutumia sarafu moja hapo Januari mosi.

Croatia kubadili sarafu yake na kwenda Euro itakuwa chini ya muongo mmoja baada ya Jamhuri ya zamani ya Yugoslavia ilipojiunga na Umoja wa Ulaya na kuweka hatua mpya katika ushirikiano zaidi wa umoja huo.

Afisa mkuu wa EU alisema Croatia ilitimiza masharti magumu ya kuwa sehemu ya sarafu moja ikiwa ni pamoja na kuweka mfumuko wa bei katika kiwango sawa na wenzao wa EU na pia kukumbatia matumizi ya umma.

Kujiunga na sarafu moja kutafanya uchumi wa Croatia kuwa na nguvu na kuleta manufaa kwa raia wake, wafanyabiashara, na jamii kwa jumla, Rais wa Tume ya Ulaya Ursula von der Leyen alisema. Kuipitisha Croatia kutumia sarafu ya Euro kutaifanya euro kuwa na nguvu zaidi aliongeza von der Leyen.

The post Tume ya Umoja wa Ulaya imesema Croatia imetimiza vigezo vyote kujiunga na EU appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/xr56wH4

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT