Skip to main content

TANZANIA YAPOTEZA MBELE YA ALGERIA


TIMU ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars inayonolewa na Kocha Mkuu,Kim Poulsen leo Juni 8,2022  imeambulia kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa Timu ya Taifa ya Algeria katika mechi ya pili ya kufuzu kushiriki fainali za mataifa ya Afrika AFCON zinazotarajiwa kufanyika 2023 nchini Ivory Coast.

Ndani ya dk 40 Stars iliweza kujilinda lakini makosa katika dk ya 45 liliweza kuwapa nafasi Algeria kupachika bao la kuongoza muda mfupi kabla ya mapumziko kwa bao la Amir Selmane.

Kipindi cha pili Poulsen aliweza kufanya mabadiliko kwa  kuwaingiza Kibu Dennis, George Mpole, Kelvin John na Salum Abubakar huku waliotoka ikiwa ni Feisal Salum,Simon Msuva,Nickosn Kibabage na Novatus Dismas.

 Wakati Stars ikiwa na matumaini ya kupata bao la kuweka mzani sawa dk ya 89, waliweza kufungwa kwa shambulizi la kushtukiza kupitia kwa Mohamed El Amine ambaye alianzia benchi.

Poulsen aliweka wazi kwamba kulikuwa na ugumu wa kuweza kupambana na wachezaji bora na imara hivyo ni moja ya somo ambalo watalifanyia kazi.

The post TANZANIA YAPOTEZA MBELE YA ALGERIA appeared first on Saleh Jembe.

The post TANZANIA YAPOTEZA MBELE YA ALGERIA appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/22561/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT