Skip to main content

Serikali yaitaka TWCC kuwafikia wanawake waliko vijijini

Na Faraja Masinde, Mtanzania Digital

Serikali imeitaka Taasisi ya Chama cha Wanawake wafanya Biashara Tanzania (TWCC), kuhakikisha inakuwa mstari wa mbele katika kuwafikia wanawake walioko vijijini ambao wamekuwa wakipitwa na fursa mbalimbali kutokana na mazingira yao hali inayo dumaza jitihada za kumkomboa mwanamke.

Mwenyekiti wa TWCC Taifa, Mercy Silla akizungumza alipokuwa akitoa hotuba yake ya utangulizi kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Mhe. Waziri, Dk. Doroth Gwajima kuzungumza

Agizo hilo limetolewa Dar es Salaam Juni 9, 2022 na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dk. Dorothy Gwajima wakati wa uzinduzi wa Ripoti ya Ushiriki wa Makundi Maalum kwenye Manunuzi ya Umma.

Dk. Gwajima amesema serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan, imekuwa mstari wa mbele kuandaa mazingira wezeshi ya kumkomboa mwanamke lakini fursa nyingi zimekuwa zikibakia kwa wachache waliopo mijini na kundi kubwa ambalo linafikia asilimia kubwa ya uzalishaji mali katika shughuli za kilimo likibaki bila taarifa sahihi.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dk. Dorothy Gwajima, akizindua Ripoti ya ushiriki wa Makundi Maalum katika Manunuzi ya Umma uliofanyika kwenye Hoteli Sheraton jijini Dar es Salaam.

“Nitoe wito sasa kwa ndugu zangu wa TWCC, kwakuwa ninyi tayari mnamtandao mpana uliopo nchi nzima, mtumie fursa hiyo kuwafikia wanawake waliowengi ambao wapo maeneo ya vijijini hawa bado fursa nyingi hawazifahamu.

“Hivyo mkitumia vizuri jukwaa lenu la TWCC, naimani wengi watapata mwamko na kushiriki katika mambo mbali mbali mathalani haya ya zabuni,” amesema Dk. Gwajima.
Aidha, Dk. Gwajima ameeleza kuwa serikali imeendelea kuweka mazingira mazuri ya kuwezesha wanawake kiuchumi.

“Uwepo wa mifuko rasmi ya uwezeshwaji kiuchumi ikiwemo mfuko wa maendeleo ya wanawake (WDF), TASAF, Mfuko wa Rais wa Uwezeshaji na mifuko mingine ni kielelezo kuwa serikali inawajali wanawake.

“Mwaka 2016 serikali ilifanya mabadiliko ya Sheria ya Manunuzi ya Umma ya Mwaka 2011 katika Kifungu cha 64 (a) katika kipengele cha 2 kwa kutoa nafasi kwa makundi maalum kuwezeshwa kushiriki katika fursa za manunuzi ya umma iliyotaka kutengwa asilimia 30 ya bajeti yake kwa ajili ya makundi maalum wakiwepo wanawake,” amesema Dk. Gwajima.

Mkurugenzi wa TWCC Mwajuma Hamza akizungumza alipokuwa akitoa ukaribisho kwa mgeni rasmi na wadau mbalimbali walishiriki Kikao hicho.

Upande wake Mwenyekiti wa (TWCC) Taifa, Mercy Silla ameipongeza serikali na kuomba jitihada hizo ziongezwe kwani wanawake walio wengi wanachukua mikopo wakiwa hawana maarifa ya biashara au shughuli wanayotaka kuifanya hivyo kuishia kufilisika.

“Kwanza kabisa tunampongeza Rais wetu Samia Suluhu Hassan kwa kuonyesha jitiahada za makusukudi na kwa vitendo za kutaka kuona wanawake wa Kitanzania wanajikomboa kiuchumi ikiwa ni pamoja na kutoa fursa mbalimbali zikiwemo mikopo ya Halmashauri.

“Mheshimiwa Waziri pamoja na washiriki bado ipo changamoto kwa wanawake wanaochukua mikopo ikiwepo masharti ya kukopa ambayo husisitiza kuwa kikundi cha watu jambo hili kwa namna moja linakwamisha jitihada za mtu mmoja mmoja, kwakuwa kila mtu anakuwa na mawazo tofauti hivyo hata wakichukua Mikopo wanashindwa kuelewana, lakini kama masharti yatabadilika itawezesha kila mwenye wazo lake ataweza kufanya anachoweza,” amesema Silla.

The post Serikali yaitaka TWCC kuwafikia wanawake waliko vijijini appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/8Nr5EYB

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT