Skip to main content

Russia yakabidhi kwa Kyiv maiti 210 za wapiganaji wa Ukraine

Raia wengi wa Ukraine walizuiliwa kwenye kiwanda cha chuma cha Azovstal kwa wiki kadhaa wakati Russia ikijaribu kuuteka mji huo wa Mariupol.

Wanajeshi wa Ukraine hatimaye walijisalimisha mwezi uliopita na kuwekwa mbaroni na Russia.

“Mchakato wa kurejesha maiti za wanajeshi waliofariki wakilinda Mariupol unaendelea. Kufikia sasa, maiti 210 za wanajeshi wetu zimerejeshwa, wengi wao ni walinzi mashuja wa Azovstal,” idara ya ujasusi ya wizara ya ulinzi ya Ukraine imesema kwenye Twitter.

Kumekuwa na habari chanya juu ya hatma ya walinzi wa kiwanda cha Azovstal wanaokadiriwa kuwa 2,000, Kyiv inataka wote wakabidhiwe katika ubadilishanaji wa wafungwa, lakini baadhi ya wabunge wa Russia wanataka baadhi ya wanajeshi wa Ukraine wafikishwe mahakamani.

“Kazi inaendelea kuwarejesha nyumbani walinzi wote wa Ukraine waliotekwa nyara,” idara hiyo ya ujasusi imesema.

Wiki iliyopita, ubadilishanaji wa maiti 160 kati ya Russia na Ukraine ulitangazwa na wizara ya Ukraine ya kuunganisha eneo lililokaliwa kwa muda.

The post Russia yakabidhi kwa Kyiv maiti 210 za wapiganaji wa Ukraine appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/22291/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT