Skip to main content

Rais wa Senegal na mwenyekiti wa AU aisihi Ukraine kutegua mabomu ya ardhini kurahisisha usafirishaji wa nafaka

Uvamizi wa Russia dhidi ya Ukaine na vikwazo vya nchi za magharibi dhidi ya Russia vilikwamisha usambazaji wa nafaka kutoka nchi hizo mbili, na kuzua hofu ya njaa kote ulimwenguni.

Bei ya nafaka barani Afrika, ilipanda kwa sababu ya kukwama kwa usafarishaji wa bidhaa hiyo, na hivyo kuongeza athari za mizozo na mabadiliko ya hali ya hewa na kuzua hofu ya machafuko ya kijamii.

Ikiwa usafirishaji wa ngano kutoka Ukraine hatuanzishwa, Afrika “ itakuwa katika hali ya njaa kali sana ambayo itavuruga usalama wa bara hilo,” Sall ameviambia vyombo vya habari vya ufaransa France 24 na RFI.

Russia na Ukraine zinazalisha asilimia 30 ya ngano yote ya dunia.

Moscow iliiomba Ukraine kutegua mabomu ya ardhini kwenye maji yanayozunguka bandari ya Odesa inayodhibitiwa na Ukraine ili kuruhusu usafirishaji wa nafaka, lakini Ukraine ilikataa kwa kuhofia shambulio la Russia.

Sall amesema Rais wa Russia Vladimir Putin ambaye alikutana naye wiki iliyopita nchini Russia, alimuhakikishia kwamba hilo halitatokea.

“Nilimwambia, Waukraine wanasema hata wakitegua mabomu, utaingia kwenye bandari. Alisema hapana, sitaingia, na hiyo ni ahadi aliyotoa,” rais wa Senegal amesema.

Sall anakutana na rais wa Ufaransa Emmanuel Macron leo Ijumaa.

The post Rais wa Senegal na mwenyekiti wa AU aisihi Ukraine kutegua mabomu ya ardhini kurahisisha usafirishaji wa nafaka appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/P4F1dhi

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT