Skip to main content

Rais wa Malawi ampokonya mamlaka yote makamu wake kufuatia kashfa ya ufisadi

Uchunguzi ulioendeshwa na taasisi ya kupambana na ufisadi (ACB) kuhusu undanganyifu wa zabuni umehitimisha kuwa maafisa wa umma 53 wa sasa na wa zamani walipokea pesa kutoka kwa mfanyabiashara raia wa Uingereza mwenye asili ya Malawi Zuneth Sattar, kati ya mwezi Machi na Oktoba 2021, Chakwera amesema.

Sattar anafanyiwa uchunguzi nchini Uingereza na Malawi juu ya tuhuma za ufisadi, udanganyifu na utakatishaji wa fedha.

Kulingana na katiba ya Malawi, Chakwera hawezi kumsimamisha kazi au kumfukuza kazi Chilima kwa sababu ni afisa aliyechaguliwa.

“La muhimu nachoweza kufanya kwa sasa, ni kumuweka kando na kumpokonya makujumu yote wakati nikisubiri taasisi ya kupambana na ufisadi ithibitishe tuhuma zinazomkabili,” amesema Chakwera.

Chilima hakutoa maelezo mara moja juu ya uamuzi huo. Alishirikiana na Chakwera kushinda uchaguzi wa rais wa 2020 katika muungano wa kupambana na ufisadi.

Katika hotuba kwa taifa, Chakwera alimfukuza kazi pia mkuu wa polisi George Kainja, ambaye alisikika kwenye mkanda uliorikodiwa akijadili mikataba na Sattar.

The post Rais wa Malawi ampokonya mamlaka yote makamu wake kufuatia kashfa ya ufisadi appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/26466/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT