Skip to main content

Rais Biden amelihutubia taifa akiliomba bunge kuidhinisha sheria kudhibiti vifo vya bunduki

Rais wa Marekani Joe Biden ametoa hotuba huko White House alhamis usiku kwa kulitaka bunge kuidhinisha sheria za kawaida ili kujaribu kuzuia matukio ya hivi karibuni ya vifo vinavyotokana na ufyatuaji risasi wa umma ambavyo vimewashtua wamarekani wengi.

White House imesema Biden alitoa wito wa masharti mapya ili kukabiliana na janga la ghasia za bunduki ambazo zinasababisha vifo kila siku.

Haikuwa wazi kama Biden atatetea masharti yoyote maalum ambavyo angependelea yapitishwe, kama vile ukaguzi unaoangalia historia ya nyuma kwa wanunuzi wa bunduki, au kupiga marufuku uuzaji wa silaha zenye nguvu ya haraka, ambazo zilikuwa zimetumika katika ufyatuaji risasi wa umma wa hivi karibuni.

Hakuna kipengele chochote kitakachoweza kupitishwa katika bunge lililogawanyika kisiasa ambapo wabunge kwa miaka mingi wamekuwa wakitofautiana kuhusu sheria ya kumiliki bunduki.

Lakini baadhi ya wabunge wanajaribu kuweka masharti zaidi baada ya kesi tatu za ufyatuaji risasi wa umma ndani ya kipindi cha mwezi mmoja uliopita.

Watu weusi 10 kwenye duka la vyakula waliuawa kwa kupigwa risasi katika shambulizi la ubaguzi wa rangi kwenye mji wa Buffalo katika jimbo la New York, wanafunzi 19 na waalimu wawili waliuawa kwa risasi wakiwa darasani mwao katika shule ya msingi ya Robb kwenye mji wa Uvalde katika jimbo la Texas, na watu wanne wengine waliuawa katika kituo cha matibabu cha Tulsa katika jimbo la Oklahoma.

The post Rais Biden amelihutubia taifa akiliomba bunge kuidhinisha sheria kudhibiti vifo vya bunduki appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/ux4qdYc

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT