Skip to main content

Raia takribani 100 wameuawa kaskazini mwa Burkina Faso; vyanzo vya usalama vimesema

Watu wenye silaha waliwaua takribani raia 100 katika wilaya ya mashambani kaskazini mwa Burkina Faso karibu na mpaka na Niger mwishoni mwa wiki chanzo cha usalama kilisema.

Washambuliaji waliwalenga wanaume lakini walionekana kuwaachia wanawake na watoto katika wilaya ya Seytenga Jumamosi usiku chanzo cha usalama na vyanzo vingine viwili vilisema wote wakizungumza kwa sharti la kutotajwa majina.

Hakuna kundi lililodai kuhusika na shambulizi lakini inaelezea shambulizi hilo lilitokea katika maeneo ya mpakani ambako wanamgambo wanaohusishwa na al-Qaida na Islamic State wanaendesha uasi wao huko.

Takribani watu 3,000 waliokimbia shambulizi hilo wamewasili Dori mji mkuu wa Burkina Faso katika eneo la Sahel ambako mashirika ya misaada yapo kwenye eneo alisema afisa wa eneo hilo ambaye aliomba jina lake lisitajwe.

Kulikuwa na taarifa tofauti juu ya idadi ya vifo. Afisa huyo wa usalama alisema siku ya Jumatatu kwamba takribani watu 100 walikufa. Chanzo katika eneo hilo ambacho hakikutaka kutajwa jina kilisema kwamba idadi ya watu waliokufa ilikuwa 165.

The post Raia takribani 100 wameuawa kaskazini mwa Burkina Faso; vyanzo vya usalama vimesema appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/24043/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT