Skip to main content

Mwana Mfalme wa Saudi Arabia amekutana na viongozi wa Misri, Jordan na Uturuki kuboresha ushirika

Mtawala mkuu wa Saudi Arabia mwana mfalme Mohammed bin Salman alikutana rasmi na viongozi wa Misri, Jordan na Uturuki wiki hii. Lengo lake wanasema wachambuzi ni kuunganisha nafasi zao katika masuala ya usalama kama vile wasiwasi unaoongezeka juu ya Iran. Kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kuimarisha uhusiano wa nchi mbili na Saudi Arabia mzalishaji mkuu wa mafuta. Ilikuwa sehemu ya ziara hiyo wachambuzi wanasema huku janga la COVID-19 na uvamizi wa Russia nchini Ukraine unaendelea kuwa na athari kubwa.

Ziara ya mwana mfalme wa Saudi Arabia, Mohammed bin Salman wiki hii katika eneo hilo, wachambuzi wanasema inaashiria azma yake ya kutambuliwa katika jukwaa la ulimwengu na kumaliza miaka kadhaa ya kutengwa kimataifa kufuatia mauaji ya mwaka 2018 na kukatwakatwa kwa mkosoaji wa Saudi Arabia, Jamal Khashoggi mjini Istanbul ambapo mkuu huyo amekanusha kuhusika binafsi.

Rais wa Marekani Joe Biden aliitaja Saudi Arabia kama isiyo na ushawishi wakati alipofanya kampeni lakini nchi hizo mbili ni washirika wa kihistoria.

Mchambuzi raia wa Jordan, Al Sabaileh ameiambia VOA kwamba vita vya Russia nchini Ukraine, vimesukuma kupanda kwa bei ya mafuta na kusababisha uhaba wa chakula duniani, vimefungua kwa Saudi Arabia mabadiliko katika sheria za ushirikiano na utawala wa Marekani. Saudi Arabia ndio muuzaji mkubwa wa mafuta duniani.

Mchambuzi katika kituo cha Stimson chenye makao yake Washington, Al Sabaileh anasema kwamba ushiriki wa Rais Biden katika mkutano wa Julai 16 huko Jeddah unaowakutanisha pamoja viongozi wa nchi sita za baraza la ushirikiano wa Ghuba (GCC) pamoja na wale kutoka Jordan, Misri na Iraq unampa Bin Salman kama anavyojulikana MBS hadhi fulani na uwezo wa kusaidia kuweka ajenda ya kikanda hasa kwa Iran na Israel. Saudi Arabia ni mmoja wa wanachama wa GCC.

Marekani iliafiki makubaliano ya Abraham mwaka 2020 na kuhalalisha uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi kati ya Israel na mataifa ya Ghuba ya Umoja wa falme za kiarabu na Bahrain. Hakuna nchi iliyowahi kuwa na vita na Israel, tofauti na Misri na Joedan ambazo zilitia saini mikataba ya Amani na taifa la kiyahudi mwaka 1979 na 1994.

The post Mwana Mfalme wa Saudi Arabia amekutana na viongozi wa Misri, Jordan na Uturuki kuboresha ushirika appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/27576/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT