Skip to main content

Mkuu wa zamani wa kijasusi Afrika kusini awasilisha mashtaka dhidi ya Rais Ramaphosa

Mkuu wa zamani wa kijasusi nchini Afrika kusini Arthur Fraser alisema Jumatano kwamba aliwasilisha malalamiko ya kisheria dhidi ya Rais wa Afrika kusini Cyril Ramaphosa akimtuhumu kuteka nyara na kuwahonga majambazi walioiba mamilioni ya dola kutoka kwa moja ya mali zake.

“Nimechukua hatua ambayo haijawahi kushuhudiwa ya kufungua mashtaka ya jinai dhidi ya mheshimiwa, Rais wa Jamhuri ya Afrika kusini, Cyril Ramaphosa” mkuu wa zamani wa ujasusi Arthur Fraser alisema katika taarifa.

Kulingana na Fraser ni kwamba wezi hapo Februari tisa mwaka 2020 walivamia shamba kaskazini mwa Johannesburg mali ya Rais Ramaphosa kwa msaada wa mfanyakazi wa ndani ambapo walifanikiwa kuiba zaidi ya dola milioni nne.

Fraser amemshutumu Ramaphosa kwa kuandaa utekaji nyara wa washukiwa, kuhojiwa kwao kuhusu mali yake, pamoja na hongo. Rais Ramaphosa alificha uhalifu kwa idara ya huduma ya polisi ya Afrika kusini au idara ya mapato ya Afrika kusini na baada ya hapo akawalipa wahalifu kwa kukaa kwao kimya alisema mkuu huyo wa zamani wa kijasusi huko Afrika kusini, Arthur Fraser.

The post Mkuu wa zamani wa kijasusi Afrika kusini awasilisha mashtaka dhidi ya Rais Ramaphosa appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/xr56wH4

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT