Skip to main content

Maseneta Marekani wametangaza muundo wa pande mbili unaohusu umiliki wa bunduki

Maseneta wametangaza muundo wa pande mbili siku ya Jumapili katika kujibu mashambulizi ya bunduki kwa umma ya mwezi uliopita ikiwa mafanikio ya kawaida yanayotoa hatua za udhibiti wa bunduki na kuongeza juhudi za kuboresha usalama katika shule na program za afya ya akili.

Pendekezo hilo lipo kwenye hatua kali zilizoangaziwa kwa muda mrefu na Rais wa Marekani Joe Biden na wa-Democrat wengi. Hata hivyo kama makubaliano haya yatapelekea kupitishwa kuwa sheria inaweza kuashiria mabadiliko kutoka mauaji ya bunduki ya miaka kadhaa ambayo yameleta mwamko kidogo kutokana na kukwama katika bunge.

Viongozi wanatarajia kusukuma haraka makubaliano yoyote kuwa sheria wakiwa na matumaini itakuwa mwezi huu kabla ya kasi ya kisiasa kufifia ambayo imechochewa na ufyatuaji risasi wa umma wa hivi karibuni katika mji wa Buffalo katika jimbo la New York na jingine mji wa Uvalde katika jimbo la Texas.

Katika hatua iliyoonekana kama maendeleo makubwa maseneta 20 wakiwemo 10 kutoka chama cha Republican walitoa taarifa ya kupitishwa. Huenda hiyo ni ishara muhimu kwa sababu kikwazo kikubwa zaidi cha kupitishwa kwa hatua hiyo pengine ni katika baraza la seneti ambapo kila upande una viti 50 kwa 50 na hivyo zinahitajika kura 10 za wa-Republican kufikia kiwango cha kawaida cha kura 60 ili mswaada uweze kuidhinishwa.

The post Maseneta Marekani wametangaza muundo wa pande mbili unaohusu umiliki wa bunduki appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/23781/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT