Skip to main content

Mahakama ya Senegal ilimhukumu kiongozi wa waasi kifungo cha maisha jela kwa mauaji

Mahakama nchini Senegal Jumatatu ilimhukumu kiongozi mtoro wa waasi na wanaume wengine wawili kifungo cha maisha jela kwa mauaji pamoja na uasi wa kutumia silaha kutokana na mauaji yaliyogharimu maisha ya watu 14.

Cesar Atoute badiate mkuu wa Movement of Democratic Forces of Casamance (MFDC) kundi la waasi linalopigania uhuru katika eneo la kusini mwa Senegal alihukumiwa bila yeye kuwepo kufuatia mauaji hayo.

Omar Ampoi Bodian mwanachama mwingine wa kundi hilo na mwandishi wa habari Rene Captain Bassene walipewa hukumu hiyo-hiyo wakili wao Cire Cledor Ly aliliambia shirika la habari la AFP.

Mahakama ya Ziguinchor katika jiji kuu la Casamance ilitoa hukumu zilizosimamishwa kwa miezi sita kwa washtakiwa wengine wawili na kuwaachilia wengine 11. Kesi hizo zilitokana na tukio la Januari sita mwaka 2018 ambapo wanaume 14 walifungwa kamba na kuuawa wakati walipokuwa wakienda kukata kuni katika msitu uliohifadhiwa karibu na Ziguinchor.

Wapiganaji wa waasi wa Casamance walitumia msitu huo kama kituo na mamlaka ya Senegal inawashutumu kwa kufadhili shughuli zao na kusafirisha kuni pamoja na bangi. Kundi hilo la waasi lilikanusha kuhusika kwa vyovyote vile likiwashutumu maafisa wa serikali kwa ufisadi.

The post Mahakama ya Senegal ilimhukumu kiongozi wa waasi kifungo cha maisha jela kwa mauaji appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/24039/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT