Skip to main content

Ma rais kadhaa wasusia mkutano wa nchi za Amerika unaofanyika Los Angeles, California

Mkutano huo utasusiwa na ma rais wa Guatemala, Honduras na Mexico na wengine kama njia ya kupinga uamuzi wa Washington wa kuzitenga kwenye mkutano huo serikali za Cuba, Nicaragua na Venezuela.

Kutokuwepo ma rais sita tayari imeleta dosari kwenye mkutano wa kilele unaoangaliwa kama fursa kubwa ya kushughulikia changamoto zinazolikabili eneo hilo, ikiwa ni pamoja na ukosefu wa usalama wa kiuchumi, afueni baada ya janga la covid, mabadiliko ya hali ya hewa, uhamiaji na mgawanyiko wa kisiasa.

Ukikabiliwa na shinikizo la kisiasa ndani ya nchi, ikiwemo lile la jamii zilizo uhamishoni katika jimbo la Florida, utawala wa Biden uliamua kwamba Cuba, Nicaragua na Venezuela hazikidhi vigezo vya mkataba wa 2011 wa kidemokrasia kati ya nchi za Amerika ambao unasisitiza demokrasia kama jambo la msingi.

Washington ilitangaza rasmi kwamba nchi hizo zimeondolewa kwenye orodha ya washiriki, tarehe 5 Juni, siku moja kabla ya hafla hiyo kuzinduliwa.

The post Ma rais kadhaa wasusia mkutano wa nchi za Amerika unaofanyika Los Angeles, California appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/22293/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT