Skip to main content

Kipindupindu kimeibuka tena Cameroon na kusababisha vifo takribani 150

Zaidi ya watu 150 wamefariki kutokana na kuibuka tena kwa ugonjwa wa kipindupindu nchini Cameroon katika kipindi cha miezi minane iliyopita Umoja wa Mataifa ulisema Jumatatu.

Wizara ya afya ya Cameroon iliandikisha kesi 8,241 na vifo 154 hadi mwisho wa mwezi mei, ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masuala ya kibinadamu (OCHA) ilisema.

Mikoa saba kati ya 10 ya taifa hilo la Afrika magharibi wameripoti kesi za kipindupindu. Mikoa iliyoathirika zaidi ni mikoa inayotumia lugha ya kiingereza, huko kusini-magharibi ikiwa na kesi 5,628 na vifo 90 ikifuatiwa na wilaya ya Littoral yenye kesi 2,208 na vifo 58 OCHA ilisema.

Fursa ya kufika kusini-magharibi bado ni ngumu sana baada ya miaka mingi ya ghasia kati ya watu wanaotaka kujitenga wanaotumia lugha ya Kiingereza na jeshi, alisema mkuu wa OCHA ofisi ya Cameroon, Karen Perrin.

Kipindupindu ni ugonjwa wa kuharisha ambao unatibika kwa dawa za Antibiotic na kunywa maji kwa wingi lakini ugonjwa unaweza kuua ndani ya saa chache kama usipotibiwa.

Milipuko hutokea mara kwa mara huko Cameroon ambapo kuna wakaazi zaidi ya milioni 25. Janga la mwisho la kipindupindu lilitokea kati ya Januari na Agosti mwaka 2020 ambapo watu 66 walikufa.

The post Kipindupindu kimeibuka tena Cameroon na kusababisha vifo takribani 150 appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/24041/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT