Skip to main content

Kikosi cha nchi nne za Afrika magharibi kinasema kimewaua wanamgambo wa kiislamu 805

Nchi hizo nne za Afrika magharibi pamoja na Benin ziliunda kikosi hicho mwaka wa 2015 kupambana na kundi la Boko Haram na hasimu wake, the Islamic State in West Africa Province ( ISWAP).

Kikosi kazi hicho cha mseto (MNJTF) kimesema wanamgambo wa kiislamu 805 waliuawa kwenye visiwa vya ziwa Chad na maeneo jirani kati ya tarehe 28 Machi na tarehe 4 Juni, wakiitaja operesheni hiyo kuwa yenye maafanikio.

Bonde kubwa la Ziwa Chad linavuka mipaka ya Nigeria, Niger, Cameroon na Chad, Boko Haram na ISWAP waliweka ngome zao kwenye visiwa vyake vingi vidogo.

Takriban wanajeshi 3,000 kutoka nchi hizo nne walihusika katika opereheni hiyo na kuteka au kuharibu magari 44, pikipiki 22 na silaha, uwanjani, kwenye bahari na katika operesheni za anga, kikosi hicho kimesema.

Risasi zilikamatwa na vituo vya kutengeneza vilipuzi vilivyoboreshwa viliharibiwa, kikosi hicho kimesema.

Kikosi hicho kimeongeza kuwa wanajeshi 20 kutoka Niger walijeruhiwa, na mmoja yuko katika hali mbaya.

The post Kikosi cha nchi nne za Afrika magharibi kinasema kimewaua wanamgambo wa kiislamu 805 appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/22299/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT