Skip to main content

Jeneza la mabaki ya Lumumba lawasili DRC kwa ajili ya mazishi

Ndege ilichukua mabaki ya Lumumba, hasa jino ambalo Ubelgiji, mkoloni wa zamani wa Congo, ilikabidhi kwa familia yake Jumatatu, kutoka Brussels hadi Kinshasa, mabaki hayo yatasifirishwa kote nchini DRC kwa siku tisa.

Jeneza na wajumbe walioandamana nalo walisafiri kwa ndege hadi mkoa wa kati wa Sankuru, ambako kiongozi huyo wa kwanza wa nchi hiyo baada ya uhuru alizaliwa katika kijiji cha Onalua mwaka wa 1925.

“Mheshimiwa waziri mkuu wangu wa kwanza, polisi na wanajeshi wa DRC wamejipanga kukupa heshima zao ukirejea kijijini mwako,” afisa wa polisi aliyesimama kwa umakini amesema, mbele ya jeneza lilipowasili kwenye uwanja wa ndege katika mji wa Tshumbe.

Kutoka hapo, lilipelekwa kilomita 25 hadi Onalua, ambako siku mbili za kutoa heshima zimepangwa.

Mabaki hayo yatapelekwa kwenye maeneo muhimu kwa maisha ya Lumumba na kuzikwa katika kaburi mjini Kinshasa tarehe 30 mwezi huu, kufuatia siku tatu za maombolezo ya kitaifa.

The post Jeneza la mabaki ya Lumumba lawasili DRC kwa ajili ya mazishi appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/27084/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT