Skip to main content

GEITA GOLD YAFUNGIWA NA FIFA KUSAJILI


SHIRIKISHO la Kimataifa la Soka (FIFA) limeifungia Klabu ya Geita Gold kusajili wachezaji hadi itakapomlipa aliyekuwa kocha wa timu hiyo Ettiene Ndayiragije.

Kocha huyo raia wa Burundi alifungua madai dhidi ya Geita Gold akidai fidia ya kuvunjiwa mkataba pamoja na malipo mengine wakati akiifundisha timu hiyo ya mkoani Geita.

Kwa mujibu wa taratibu za FIFA, iwapo Geita itakuwa haijamlipa kocha huyo suala hilo litawasilishwa katika Kamati ya Nidhamu ya FIFA kwa ajili ya hatua zaidi za kinidhamu.

Taarifa ambayo imetolewa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)imeweka bayana kwa  kuzikumbusha klabu kuheshimu mikataba ambayo zinaingia na wachezaji pamoja na makocha, kwani hiyo ni moja ya vigezo vya kupata Leseni ikiwa ni utekelezaji wa Kanuni ya Leseni za Klabu (Club Licensing Regulations).

Kwa sasa Geita Gold ipo chini ya Felix Minziro ambaye anakinoa kikosi hicho chenye mzawa namba moja kwa utupiaji ambaye ni George Mpole mwenye mabao 16.

The post GEITA GOLD YAFUNGIWA NA FIFA KUSAJILI appeared first on Saleh Jembe.

The post GEITA GOLD YAFUNGIWA NA FIFA KUSAJILI appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/z2IZnL9

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT